Monday 21 December 2009

Yanga na Simba kukipiga Taifa Mpya nusu fainali ya Tusker

Shirikisho la soka hapa nchini (TFF) kwa kushirikiana na waandaaji wa michuano ya kombe la Tusker wamesema mchezo wa nusu fainali ya pili ya michuano hiyo baina ya watani wa jadi wa soka la Tanzania Yanga na Simba utapigwa kwenye dimba la Taifa (Shamba la babu).
Pamoja na kusema hivyo TFF imeweka wazi viingilio vya mchezo huo ambayo hazina tofauti na michezo mingine ya timu hizo mbili zinapokutana kwenye michuano mbali mbali.
Kiingilio cha juu siku hiyo ni elfu 40 huku kiingilioa cha chini kikiwa ni elfu 5.
Mchezo huo wawatani wa jadi utapigwa siku ya Alhamis Desemba 24 siku moja kabla ya sikuku ya xmass, mchezo huo utatanguliwa na mchezo baina ya wakenya watupu timu za Sofabaka na Tusker.
Msemaji wa TFF- Florian Kaijage amesema kuwa wao walishindwa kusema mapema kuwa mchezo huo utachezwa kwenye dimba la Taifa kwasababu uwanja huo unamilikiwa na Serikali lakini sasa kila kitu kipo safi.

No comments: