Tuesday 1 May 2007

SIMBA WASHINDWA KULIPA HOSTEL MORO

Ama kwa hakina mpenzi wa soka huwezi kuamini timu ya Simba imeshindwa kulipa kiasi cha shilingi 140000 za kitanzania kwa ajiri ya kulipia Hostel waliyokuwa wakikaa kwa kipindi cha wiki mbili za mashindano ya ligi ndogo ya TFF
Habari kutoka Morogoro zinasema kwamba wachezaji wa timu hiyo waliluhusiwa kuondoka kwenye Hostel za chuo kikuu cha Waislamu mkoani humo lakini gari la kingozi mmoja wa timu hiyo ya Simba aina ya Toyota Prado namba T276ABX limezuhiliwa hadi pale viongozi wa timu hiyo ya Simba watakapolipa deni hilo
Mmoja wa viongozi wa Hostel hiyo ameuammbia mtandao huu kuwa kwa kipindi cha wiki zote mbili walizokaa pale ni wiki moja tu viongozi wa timu hiyo walilipa kodi lakini wiki nyingine moja hawakulipa kodi na walitaka kuwazuia na wachezaji wa timu hiyo wasiondoke lakini wamemua kuwaachia na kulizuia gari hilo hadi pale watakapopata pessa zao
Katika Hostel hiyo Simba walikuwa wakipata huduma mbalimbali kama vile chakula na uwanja wa kufanyia mazoezi na kila kitu walitakiwa kukilipia lakini wao hawakulipa na viongozi wa Hostel hiyo waliwaamini sana viongozi wa timu hiyo lakini hivi sasa uaminifu wao umekwisha
Hapo jana timu ya Simba walicheza mchezo wao wa mwisho wa michuano hiyo ya ligi ndogo dhidi ya Ashant United na kupokea kipigo cha bao 2-0 hivvo kumaliza michuno hiyo wakiwa wa pili nyuma ya wauza mitumba hao kutoka mitaa ya ILALA hapa Dar es salaam

John Terry atamani kuifundisha Cheslea

Nahodha wa timu ya Chelsea John Terry amesema anataka baada ya kustafu kuichezea timu hiyo basi awe kocha wa timu hiyo
John Terry ameliambia shirika la Utangazaji la Uingereza BBC kuwa anataka siku moja awe kocha wa timu ya Chelsea pale atakapo sitafu kucheza soka
Ameendelea kueleza kwamba pale alipokuwa akizungumza na viongozi wa timu hiyo kuhusu mkataba wake aliwambia wampe makataba wa miaka tisa na baada ya hapoa basi awe kocha wa timu hiyo
Sina hamu kabisa ya kuhama Chelsea kwamaana ninataka nipate mafunzo ya ukocha na baadae nije niifundisha timu hiii ninayoipenda ameeleza John Terry

Nani mtemi hii leo baina ya Liverpool na Chelsea

Ni mara nyingine tena timu mbili za nchini Uingereza za Liverpool na Chelsea zinamumaana kwenye mchezo wa marudianao wa ligi ya mabingwa barani Ulaya
Katika mchezo wa kwanza uliofanyika kwenye uwanja wa Chelsea mabilione hao walifanikiwa kuifunga Liverpool bao 1- 0,bao lilofungwa na kiungo mchambuliaji Joe Cole
Mchezo wa leo unapigwa kwenye uwanjwa wa Anfield nyumbani kwa Liverpool huku wenyeji hao wakiwa na matumaini makubwa kurudi yake walioyafanya mwaka 2005 ambapo walifanikiwa kuitoa Chelsea kwenye michuno hiyo baada ya kuinyuka baoa 1-0,bao lilotiwa kimiani na Luis Gacia
Hii leo Chelsea itaingia dimbani bila la kiungo wake rai wa Ujerumani Michael Ballack aliemajeruhi na mlinzi wa kati Ricardo Carvslho ambae nae ni majeruhi hinyo kumfanya kocha wa Chelsea Jose Mourinho kuumia kichwa
Katika hatua hiyo Mourinho atalazimika kumtumia kiungo wa Ghana Michael Essien kama m linzi wa kati akishirikia na John Terry ilikuweza kulinda ngome ya timu hiyo pamoja na kulinda ushindi wao wa goli moja walioupata nyumbani kwao
Kunauwezekana pia mshambuliaji hatari wa timu ya Chelsea raia wa Ukrain Andriy Shevchenko akaukosa mchezo wa leo kutokana na maumivu ya misuli hivyo kuzi kumuumiza Jose Mourinho
Kwa upande wa Liverpool wao hawana amatatizo kabisa kwamaana kikosi chao chote ni kizima na hakina matatizo yeyote yake
Na kocha wa Liverpool Rafael Benitez amejigamba kuwa lazima waitoe timu hiyo kwamaana wamejianda kikamilifu na wanahamu tena ya kucheza fainali ya michuno hiyo kama walivyofanya mwaka 2005

Wauza mitumba wamuua mnyama Simba

Wauza mitumba wa Ilala timu ya Ashant hapo jana walizihilisha kuwa wao ni mwamba kwa timu ya Simba baada ya kuinyuka timu hiyo bao 2-0 kwenye mchezo wa ligi ndogo ya TFF
Uzembe uliofanywa na mlinzi wa kati timu ya Simba Said Kokoo ulimpa nafasi mshambuliaji Mussa Kipao kuipatia timu yake ya Ashant United bao la kwanza katika dakika ya 18 na kuifanya timu yake iwe mbele kwa bao hilo moja hadi mapumziko
Ashant United walikomelea msumari wa moto na wa mwisho kwenye jeneza la timu ya Simba katika dakika ya 54 kupitia kwa mshambuliaji wake Patrick Mrope aliemzidi mbio mlinzi wa Simba Nurdin Bakari
Kwa matokeo hayo Ashant United imezihilisha uwamba wake kwa timu hiyo ya msimbazi kwamaana katika mchezo wa kwanza baina ya timu hizo haukumalizika baada ya mashabiki wa timu ya Simba kuanzisha vurugu na TFF ikaamuru kuipa Ashant United pont tatu na magoli mawili
Pia kwa matokeo hayo Ashant United imefanikiwa kuongoza kituo cha Morogoro kwa kuwa na point 13 na kufuatiwa na timu ya Simba yenye point 10
Timu hizo zote mbili zimefanikiwa kuingia hatua ya sita bora ambapo hivi sasa zinasubiria timu zingine nne kutoka katika vitua vya Arusha na Dodoma