Mchezo huo utachezwa siku ya Alhamis siku moja kabla ya sikuku ya X-masss kwenye dimba la Taifa (Shamba la Babu) na wachezaji ambao ni majeruhi hadi leo ni pamoja na nahodha Nico Nyagawa,Haruna Moshi Boban,Emmanuel Okwi na kiungo Uhuru Selemani ambae tayari imeshathitika kuwa hatocheza mchezo huo.
Meneja wa timu hiyo ya Simba Innocent Njovu amesema bado hawajui chochote kama wachezaji hao watacheza mchezo huo siku ya Alhamis au la ila bado wanaendelea na matibabu.
Njovu amesema mustakabali wa swala hilo litajulikanika hapo kesho kama wachezaji hao watacheza mchezo dhidi ya Yanga au hawatocheza.
No comments:
Post a Comment