Tuesday 22 December 2009

Kesho ni vita ya Wakenya kwenye Shamba la bibi

Makocha wa timu za SOFAPAKA NA TUSKER zote kutoka Kenya wametambiana kushinda katika mchezo wao wa NUSU FAINALI wa michuano ya kombe la TUSKER Mchezo utakaofanyika hapo kesho katika uwanja wa UHURU Jijini DSM.
Katika mchezo huo wa nusu fainali timu itakayoshinda itakutana katika fainali mshindi wa mchezo kati ya SIMBA au YANGA zinazotarajia kucheza alhamisi wiki hii.
Kwa upande wake kocha wa timu ya TUSKER James Nandwa amesema makosa yaliofanyika katika mchezo na YANGA hayatajirudia tena kwani wachezaji wake wamejiandaa vizuri kwa mchezo huo na wamejinda kushinda.Kocha wa mabingwa wa Kenya msimu huu timu ya Sofapaka Robert Matano amesema msimu huu Tusker ni wao na hapo kesho wanaenda kushinda tu mchezo huo sio kingine.

No comments: