Monday 21 December 2009

PST na TPBO watofautiana kuhusu mpinzani sahihi wa Cheka


Chama cha ngumi za kulipwa nchini (TPBO) kimekanusha taarifa za kuwepo kwa dhuluma katika pambano la ngumi za kulipwa ambapo bondia FRANCIS CHEKA alibadilishiwa mpinzani siku moja kabla ya pambano.
Utata mkubwa juu ya pambano hilo uliibuka mara baada ya kuwepo kwa taarifa za kutowasili kwa bondia huyo hali iliyowashitua wapenzi wengi wa masumbwi ambao walikuwa wakisubiri kwa hamu kubwa pambano hilo.
Hata hivyo pambano hilo lilifanyika ambapo FRANCIS CHEKA alipewa mpinzani toka Brazil na kumchakaza mpinzani wake huyo anaeitwa ISAACK TARAVES kwa KNOCK OUT katika raundi ya pili na kufanikiwa kutetea taji lake la IBO na WBC.
Rais wa TPBO YASSIN ABDALAH amesema kuwa uamuzi wa kubadilisha bondia ulitokana na kuchelewa kwa hati ya kusafiria ya bondia HENRIQ ARECO ambaye awali alitakiwa kupigana na Cheka.
Kauli hiyo inatofautiana na ya Rais wa shirikisho lingene la masumbwi ya kulipwa hapa nchini PST – Emmanuel Mlundwa ambae aliwambia mashabiki siku ya pambano kuwa bondia huyo hakua kwasababu ni mzee, sasa tuamini la nani … ni mzee au alikosa hati ya kusafiria…..

Wadau wa masumbwi wanadai kuwa huo ni ufisadi sasa mimi siju …

No comments: